Sunday 30 September 2012

MSIBA


MZEE SIRIKWA (PICHANI) WAKATI WA UHAI WAKE AKICHANGIA HOJA KATIKA KIAKO CHA HALMASHAURI KUU YA TAIFA NCCR- MAGEUZI.
NCCR-MAGEUZI
National Convention For Construction And Reform – Mageuzi
Taarifa kwa wanachama kupitia vyombo vya habaria
YAH: KUANGUKA KWA NDG. EMMANUEL PETRO OLE – SIRIKWA
Ndugu wanahabari,
Asubuhi ya kuamkia tarehe 28 Septemba, 2012 aliyekuwa kamishna wa Chama chetu mkoa wa Arusha, mjumbe wa  Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama, mmoja wa wajumbe wa Baraza la Wadhamini, mmoja wa waasisi wa Chama na aliyekuwa na kadi Na.3 ya NCCR-Mageuzi, Mzee Emmanuel Petro Ole- Sirikwa alifariki dunia katika hospitali ya AICC  Mkoani Arusha alikokuwa amelazwa kwa takribani majuma mawili.
Chama kimempoteza mtu muhimu, alikuwa ndiye kinara  miongoni mwa wanachama waliopewa kadi za mwanzo. Waasisi wenzake  waliokuwa na kadi Na.1 na Na. 2, misukosuko ya kijamii, kisiasa na kiuchumi  iliwafanya wamsaliti mtoto waliyemzaa (NCCR-Mageuzi) na kukimbilia vyama vingine.
Emmanuel Petro Ole- Sirikwa, hakuyumba na aliendelea kubaki ndani ya chama chake,hali iliyotufanya baadhi ya yetu kumuona kama mzee wa boma la chama.
Mzee Sirikwa alibaki ndani ya chama kwa sababu ya:

  • Kuheshimu na kuthamini kile alichokianzisha
  • Lengo na madhumuni ya kuanzisha chama hayajafikiwa
  • Uwepo wa demokrasia chanya hapa nchini bado ni kitendawili
Pamoja na haya yaliyomkuta (Mauti) sisi tuliobaki  tutaendeleza na kuyasimamia mazuri yote aliyosimamia hadi hapo malengo ya kuanzisha chama hiki yatakapotimia.
Kutokana na heshima na historia yake ndani ya chama, na vilevile ikizingatiwa kuwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu hayana makosa na wala hayawezi kukatiwa rufaa. Chama kimeamua kuenzi uvumilivu na misimamo yake kwa kuuita ukumbi wa mikutano ulioko makao makuu ya chama kwa jina la “ UKUMBI WA SIRIKWA”.
Maziko yake yanatarajiwa kufanyika Kijijini kwake Olijilah- Arumeru Mkoani Arusha tarehe 3-10-2012.
Katika maziko hayo, chama kitawakilishwa na viongozi wakuu wa chama wakiongozwa  na Ndugu James Francis Mbatia (Mb), Mwenyekiti wa Chama Taifa.
NCCR-Mageuzi inawaomba wanachama wetu, wapenzi na mashabiki kuupokea msiba huu kwa jicho chanya,na kuendeleza mazuri yote aliyoyaishi wakati wa uhai wake.
……………………………
Mussa Kombo Mussa
NAIBU KATIBU MKUU (Zanzibar)

No comments:

Post a Comment