TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: KESI YA UCHAGUZI JIMBO LA MOSHI
MJINI
Ndugu waandishi wa habari, mwaka
2010 niliteuliwa na chama changu (NCCR – Mageuzi) na baadae Tume ya Taifa ya Uchaguzi
kugombea ubunge katika jimbo la Moshi Mjini
Pamoja
na mimi, Tume pia iliwateua wagombea wa vyama vingine kugombea ubunge wa jimbo
la Moshi Mjini.
Mimi
sikuridhika na uteuzi wao, niliwawekea pingamizi baada ya kubaini kuwa uteuzi
wao ulikiuka sheria za uchaguzi, pingamizi zangu zilitupiliwa mbali, na kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi nilifungua
shauri No 1/2010 la kesi ya uchaguzi, katika Mahakama Kuu ya Tanzania kanda
ya Moshi kati ya FAUSTIN SUNGURA
dhidi ya MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI na NDESAMBURO PHILEMONI.
Mara
baada ya kufungua shauri hilo kwa mujibu wa kifungu cha 115 (1) cha sheria ya uchaguzi, nilitakiwa pia kufungua shauri la maombi N0 39/2010 juu ya dhamana ya mahakama
kama ilivyo matakwa chini ya kifungu cha 111
(3) cha sheria hiyo.(CAP 343 RE 2010).
Hata
hivyo, kesi yangu imekuwa inaendeshwa kwa upendeleo, kinyongo, lakini pia
kinyume cha sheria. Mahakama Kuu kanda
ya Moshi chini ya Jaji Moses Mzuna, imekuwa inanikandamiza na kuhakikisha ninakata
tamaa ya kudai haki yangu, ili kumpa nafasi Mhe, Ndesamburo Philemoni amalize
muda wake bila kesi yangu ya msingi kusikilizwa.
UKIUKWAJI WA SHERIA,VINYONGO NA
UPENDELEO
(1) Mnamo
tarehe 7/12 /2010 nilifungua maombi N0 39/2010 juu ya kiasi cha dhamana ya
kulipa mahakama au kusamehewa kulipa dhamana yoyote, maombi haya yalitakiwa
kutolewa uamauzi kabla ya au tarehe
21/12/2010. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 111 (3) cha sheria ya uchaguzi.
Hata hivyo, Jaji Moses Mzuna aliamua kutoa uamuzi
baada ya miezi sita (Tarehe 24/6/2011) kinyume cha sheria, lakini pia
kuhakikisha kesi inachukua muda mrefu ili kunikatisha tamaa.
(2) Mara
baada ya mahakama kuridhika kuwa sina hela, alitoa uamuzi akinieleza
kuchangisha Tshs: 8,000,000/= ndani ya siku 14 kutoka kwa marafiki zangu,
maamuzi haya ni kinyume cha kifungu cha 111(5)
(a) na (b) cha sheria ya uchaguzi (CAP
343 RE 2010), lakini pia yalilenga kuhakikisha ninakata tama ya kuendelea
na kesi yangu.
(3) Baada
ya kutoridhishwa na uamuzi huo, sheria inanipa haki ya kuomba marejeo ya uamuzi
wa Jaji, hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 78
(b) au Order XLII (1) (b) vya sheria
ya mwenendo wa mashauri ya madai (CAP 33
RE 2002), niliwasilisha maombi hayo na yalisajiliwa na kupewa namba
11/2012.
Pasipo halali na wala sheria yoyote,
Jaji alitolea uamuzi maombi hayo bila kunisikiliza, aliamua kuyafukuza
mahakamani, hii ni kinyume cha Ibara ya 13
(6) (a) ya Katiba ya nchi (Sheria
kuu/mama ya nchi)
Jaji alilenga
kunikatisha tama na kuhakikisha Mhe Ndesamburo Pholemoni anaendelea kuwa mbunge
bila kesi ya msingi kusikilizwa.
(4) Mnamo
tarehe 6/1/2012, wadaiwa wangu walipokea
hati /wito kuwasilisha nyaraka mahakamani (Summons), walitakiwa na
sheria, Amri ya VIII, kanuni ya 1 (2) na kifungu cha 5 vya sheria ya mwenendo wa kesi za
madai kusajili nyaraka zao kabla au
tarehe 28/1/2012, au kuwasilisha maombi ya kusajili nyaraka nje ya muda kabla
au tarehe 17/2/2012.
Hata hivyo, katika
kesi yangu, wagomvi wangu waliamua kusajili nyaraka zao, hati za viapo kinzani (Counter
affidavits) takribani miezi mine (4) baadae na nje kabisa ya muda, lakini Jaji Moses Mzuna akawaonea haya wagomvi
wangu na kuifumbia macho sheria na akazikubali nyaraka zilizoingizwa mahakamani
kupitia dirishani badala ya mlangoni. Yote hii ni kunifanya nikate tamaa ya
kuendelea kudai haki yangu mahakamani.
(5) Mnamo
tarehe 9/5/2012, Mhe Ndesamburo
Philemoni alisajili mahakamani hati ya kiapo kinzani (counter affidavit)., nami nilipewa nakala ya hati hiyo kutoka
mahakamani hapo. Baada ya kuipitia niligundua ina makosa makubwa ya kisheria.
Mnamo tarehe
18/5/2012 nililipia ada ya ukaguzi wa jalada (perusal fee)na kupewa stakabadhi No 41539584
Katika ukaguzi wa
jalada la mahakama linalohusiana na kesi yangu, nilikuta hati ya kiapo kinzani
(counter affidavit) ya Mhe:
Ndesamburo Philemoni inafanana na ile nakala niliyopewa mimi, na kwamba hati
hiyo ilisajiliwa mahakamani hapo tarehe 9/5/2012
kwa stakabadhi No 41539390
iliyolipiwa Tshs: 3000/= pamoja na ada ya pingamizi
Baada ya ukaguzi
huo, nilisajili pingamizi la kupinga hati ya Mhe: Ndesamburo kuendelea kubaki
kwenye kumbukumbu za mahakama kwa sababu;
(a)
Mnamo tarehe 9/5/2012 Mhe Ndesamburo
alisajili hati kinzani ya kiapo (counter
affidavit). Pasipo kufuata sheria na
kwa nia ya kumlinda na au kumsaidia Mh Ndesamburo, Jaji/ Mahakama baada ya
kuona hati hiyo ina makosa ya kisheria, alimuita kinyemela, akamrudishia hati
hizo ili akazikamilishe na kuzirudisha mahakamani siku hiyo hiyo na njia za
kinyemela.
(b)Mhe:
Ndesamburo alizipokea, lakini kutokana na majukumu mengine, au kwa uzembe
alisahau kukamilisha ufisadi huo kwa
siku hiyo na badala yake akaenda kula kiapo kesho yake (10/5/2012) na kukamilisha mapungufu yote, na bila halali na wala
kufuata utaratibu wa kisheria, akairudisha hati mahakama tarehe 10/5/2010 kinyemela.
Mnamo tarehe 14/6/2012, mahakama ilikaa kwa ajili ya; pamoja na mambo mengine, kusikiliza ufafanuzi
wa pingamizi langu juu ya hati ya kiapo kinzani ya Mhe: Ndesamburo. Baada ya
mahakama kusikiliza pingamizi hilo, ilipanga tarehe 22/6/2012 kuwa siku ya kutoa uamuzi wa pamoja na mambo mengine, juu
ya pingamizi hilo
Kabla ya kutoa
uamuzi, Mahakama au Jaji Moses Mzuna, Mhe
Ndesamburo na wakili Patrick Paul,
pasipo halali na kinyume cha kifungu cha 8 cha sheria ya Mdhibiti wa vipo (Section 8 of the Notary Public and Commissioner for Oaths )walizinyofoa hati za kiapo kinzani zilizokuwa zimekosewa,
na kinyume cha mila za mahakama na taaluma ya sheria, wakaandaa hati zingine
zinazoonyesha kwamba Mhe: Ndesamburo alikula kiapo tarehe 9/5/2012 badala ya tarehe 10/5/2012
na baadae kumpa nafasi Jaji Moses Mzuna
kuikubali hati hiyo kuwa ni halali
Jaji
Moses Mzuna, aliamua kuwalinda au kuwasaidia
mawakili wa Mhe: Ndesamburo na wale wa Serikali ili kesi ya msingi isisikilizwe
na kumpa nafasi Mhe Ndesamburo kumaliza muda wa ubunge alioupata kwa njia za
kienyeji na zisizo rasmi.
Ndugu waandishi wa
habari, maamuzi ambayo yamekuwa yanatolewa
katika Mahakama Kuu kanda ya Moshi , na ambayo hayaendani na mila za sheria, hayawezi
kukatiwa rufaa katika mahakama ya rufaa. Bali yanatakiwa kuombewa marejeo
katika mahakama kuu na iliyotoa maamuzi
hayo.
Kutokana na hali ya
upendeleo na ukiukwaji wa wazi wa sheria
kunakofanywa na Jaji Moses Mzuna na
hata kung’ang’ania kusikiliza mashauri yangu, nimejiridhisha kwamba, siwezi
kupata haki kama nitaendelea kung’ang’ania kudai haki yangu katika Mahakama Kuu
kanda ya Moshi na mbele ya Jaji Moses
Mzuna.
Kwa sababu hiyo,
nimeamua kulalamika kwa kutumia njia za kiutawala kwenye ngazi zingine zikiwemo
kwa;
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mwanasheri mkuu wa Serikali, Jaji Mkuu, Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa,
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Inspekta Jenerari wa Polisi, Mkurugenzi wa
kituo cha sheria na haki za binadamu, Jukwaa la wahariri, Ngd Philemon
Ndesamburo, Kiongozi wa balozi za nje waliopo nchini na Katibu Mkuu wa Umoja wa
mataifa (Barua zote nimezifikisha ofisi husika kati ya tarehe 9 na 17 Julai
2012).
(i)
Mkuu wa nchi - ili ajue nchi yake inavyoendeshwa
(ii)
Jaji Mkuu
– ili aitishe jalada langu na akiridhika na malalamiko yangu, anipangie majaji
watatu hadi watano wa kusikiliza kesi yangu, hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 17(1) iliyoundwa chini ya kifungu cha 11 7(1) cha Sheria ya uchaguzi.
(iii)
Mkurugezi Mkuu wa
Tasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa
- ili afanye uchunguzi wa kuona kama rushwa ndiyo inamfanya Jaji msomi kuacha kufuata sheria na kutoa maamuzi kwa
kadiri invyowapendeza wagomvi wangu.
(iv)
Insekta Generali wa
Polisi - ili kitengo cha polisi kizifanyie
uchuguzi hati za kiapo za Mhe: Philiemon Ndesamburo (ile iliyo ndani ya jalada
la mahakama na ile niliyonayo mkononi) kama zote zilisainiwa na Mhe Ndesamburo
pamoja na wakili Patrick Paul wa Moshi au kama mimi nimegushi saini ya Mh,
Ndesamburo na ile ya wakili Patrick Paul pamoja na mhuri wa pfisi ya wakili
huyo, vilevile kama nimegushi mhuri wa Mahakama Kuu kanda ya Moshi pamoja na
saini ya karani wa Mahakama hiyo, baada
ya uchunguzi achukue hatua zinazofaa na bila kujali nani ni nani.
(v)
Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa, kwa sababu Tanzania ni mwanachama wa umoja
huo.
(vi)
Jukwa la wahariri
– ili kutoa nafasi kwa watanzania wenzangu na hasa maskini, kujua kinachoendelea na hata ikiwezekana
tuunganishe nguvu zetu pamoja kutetea ustawi wa utawala wa sheria.
Nimeandika pia
katika kuenzi maneno ya busara na ustawi wa haki ya baba wa taifa, Marehemu
Julius Kambarage Nyerere kwamba, “kuna kazi katika jamii zinawezwa kufanywa
na watu wasio na nidhamu, na wanaoweza kutiliwa mashaka, Jaji au Hakimu siyo
kazi inayoweza kufanywa na watu kama hao”.
Ndugu waandishi wa
habari, hatua hii niliyofikia ya kuwahabarisha jambo hili watu muhimu na
akiwemo mkuu wa nchi, ni hatua mbayo na ya mwisho wa matumaini ya kutendewa
haki na hasa kama niliowaandikia nao wataamua kuwalinda watuhumiwa wangu.
NB,
kesi yangu kwa sasa haipo mahakamani, inaweza kujadiliwa kwa uhuru.
Ninawashukuru
kwa kunisikiliza
……………… 24/7/2012
Faustin Sungura
No comments:
Post a Comment